Uzinduzi wa Kampeni ya “Muhammad Ni Nuru Kwa Ulimwengu”

Lengo la Kampeni inakusudia kuonyesha haya:

Kampeni ya ‘Muhammad ni Nuru kwa Ulimwengu’ inakusudaia kuonesha haya:

• Kabla ya kuja kwake wanadamu walikuwa wakiishi kwenye giza.

• Kuja kwake alikuja na Nuru kutoka kwa Muumba wake.

• Akawatoa watu katika giza katika mahusiano yote aina tatu :
Mahusiano baina ya mtu na nafsi yake
Mahusiano baina ya mtu na Mola wake
Mahusiano baina ya mtu na wanadamu wenzake.

• Mtume (SAAW) akawapeleka wanadamu katika nuru kwa idhini ya Mola wake.

• Leo dunia imerudia katika giza kwa kuwa muongozo aliokuja nao SAAW haumsimamii mwanadamu

• Ni wajibu kufanya kazi ili nuru ya Mtume SAAW imuangazie kila mmoja na ulimwengu leo utoke katka giza na uibebe nuru kama alivyoileta yeye

#MuhammadNiNuruKwaUlimwengu

Maoni hayajaruhusiwa.